Umwilisho • Utoto wa Yesu • Ubatizo Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu • Miujiza ya Yesu Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu • Maneno saba Kifo cha Yesu • Ufufuko wa YesuKupaa mbinguni • Ujio wa piliInjili • Majina ya Yesu katika Agano Jipya • Yesu kadiri ya historia • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia
Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji
Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa
Magharibi
Wasiosadiki Utatu
Yesu katika sanaa mbalimbali ameshika nafasi kubwa katika uchoraji, uchongaji, muziki n.k. vya milenia mbili tangu azaliwe.
Picha za Yesu Kristo zilitokeza mapema kwa namna nyingine jinsi Ukristo ulivyosogea mbali na Uyahudi uliopinga uchoraji wa Mungu na viumbe vyake kwa jumla.
Kwanza Yesu hakuchorwa, ila aliwakilishwa na ishara mbalimbali, kama vile samaki (kwa Kigiriki jina la samaki lilitumika kwa kuchukua kile herufi yake kama mwanzo wa neno zima lililomhusu: Yesu Kristo Mwana wa Mungu Mwokozi), Mchungaji mwema, Mfalme, Mwalimu.
Baadaye alianza kuchorwa kama kijana asiye na ndevu (hadi karne VI, lakini kuanzia karne IV hata akiwa na ndevu na nywele ndefu kama ilivyozoeleka zaidi baadaye.
Kutokana na mabishano ya karne VII na karne VIII kuhusu uhalali wa picha, katika Ukristo wa mashariki namna ya kumchora iliratibiwa.
Kumbe katika Ukristo wa magharibi Karne za Kati zilileta mwelekeo mpya, wa kibinadamu zaidi, hasa kwa kufuata mvuto wa imani kwa Yesu wa historia, yaani jinsi alivyoishi duniani.
Hatimaye katika Renaissance Kristo alianza kuchorwa kama kielelezo cha mtu mkamilifu hata upande wa sura.
{{cite news}}