Sikukuu za Bikira Maria ni siku za kalenda ya liturujia ya madhehebu mbalimbali ya Kikristo zilizopangwa katika mwaka wa Kanisa[1] kufanya ukumbusho wa matukio ya maisha yake na mengineyo ya historia ya Kanisa.
Sikukuu hizo zinatofautiana kadiri ya imani ya madhehebu husika[2].
Katika liturujia ya Roma, mbali ya kumtaja Mama Bikira Maria katika kila Misa wakati wa sala ya ekaristi, kuna maadhimisho kwa heshima yake. Hapa yamepangwa kulingana na kiwango cha heshima hiyo:
Tena kila Jumamosi isiyo na adhimisho maalumu, Kanisa huadhimisha kumbukumbu ya hiari ya Mama wa Mungu.