G-Unit ni kundi la muziki wa hip hop nchini Marekani lenye asili yake kamili kutoka mjini New York City. G-Unit walianza kuiteka eneo la New York ni baada ya kutoa tepu zap kadhaa mchanganyiko. Jina hili la kikundi ni kifupi cha kutaja neno Guerilla Unit na vilevile kama Gangsta Unit.[1]
Kundi lilianzishwa na na wanachama kama, 50 Cent, Lloyd Banks, na Tony Yayo ambao wote walikulia katika nyumba moja, walirapa na waliuza dawa za kulevya pamoja[2].. Wakati 50 Cent alipojipanga na kuingia mkataba studio fulani, wote Lloyd Banks na Tony Yayo wakawa wana fanya kazi za kutoa tepu zao mchanganyiko kwa bidii ili waweze kujipatia mwamko wao wenyewe. Baadaye 50 Cent aliachia ngazi katika studio ni baada ya kutandikwa risasi mara tisa mbele ya nyumba ya bibi yake mzaa mama.[3][4] Kwa upande wao, wakawa wanamwona mwenzao amezongwa na matatizo kibao.