Tungo ni neno au nomino inayotokana na kitenzi "tunga". Kutunga ni kuweka/kushikamanisha vitu pamoja kwa kutumia kitu kama kamba au uzi kwa kupitishia ndani yake. Kwa mfano, unaweza kutunga vitu kama samaki, shanga, simbi na kadhalika.
Unaposhikamanisha vitu pamoja tunapata kitu kinachoitwa utungo (mmoja) au tungo (nyingi).
Katika taaluma ya lugha (sarufi) tuna dhana hiyohiyo ya kuweka/kushikamanisha vitu pamoja, yaani kupanga/kuweka pamoja vipashio vya lugha ili kujenga kipashio kikubwa zaidi.
Neno tungo katika lugha ya Kiswahili, hasa kwa upande wa sarufi, lina maana ya neno au mpangilio wa maneno unaotoa taarifa fulani. Taarifa hiyo inaweza kuwa kamili au la. Mfano: Yeye anayesoma.... Yule anajua kuandika. Lakini lazima kuwe na mpangilio kamili katika muundo mzima wa kisarufi.
Kishazi ni tungo yenye kitenzi ambacho chaweza kujitosheleza na kukamilisha ujumbe uliokusudiwa na mzungumzaji au kuwa na kitenzi kisichoweza kujitegemea.
Kuna aina mbili za tungo kishazi nazo ni:
Kishazi huru ni kishazi kinachotawaliwa ka kitenzi kikuu, ambacho kwa kawaida hutoa ujumbe kamili usiohitaji maelezo zaidi ya kukamilisha maana.
Kishazi tegemezi ni kishazi kinachotawaliwa kwa kitenzi kisaidizi, ambacho muundo wake hukifanya kutegemea kitenzi cha kishazi huru ili kuweza kutoa ujumbe uliokusudiwa.
Kuna aina mbili za vishazi tegemezi nazo ni: