Ktesiphon katika karne za kuwa mji mkuu ulipanuka hadi kuunganishwa na mji wa Seleukia upande mwingine wa mto Hidekeli. Mara nyingi inatajwa kama "Seleukia-Ktesiphon". Mwishoni mwa karne ya 6 na mwanzoni mwa karne ya 7, iliorodheshwa kama jiji kubwa zaidi duniani.[1]
Wakati wa vita kati ya Dola la Roma na Uajemi, Ktesiphon ilitekwa mara tatu na Waroma. Baada ya uvamizi wa Waislamu mji huo ulishuka na wakazi waliondoka, kwa sababu nafasi yake kama kitovu cha utawala na uchumi ilichukuliwa na mji mpya, Baghdad.
Kati ya maghofu ya mji wa kale yako hasa mabaki ya jumba la kifalme yanayojulikana kama Taq Kasra. [2]
A. Invernizzi, "Ten Years Research in the al-Madain Area, Seleucia and Ctesiphon," Sumer, 32, (1976), 167–175.
Luise Abramowski, "Der Bischof von Seleukia-Ktesiphon als Katholikos und Patriarch der Kirche des Ostens," in Dmitrij Bumazhnov u. Hans R. Seeliger (hg), Syrien im 1.-7. Jahrhundert nach Christus. Akten der 1. Tübinger Tagung zum Christlichen Orient (15.-16. Juni 2007). (Tübingen, Mohr Siebeck, 2011) (Studien und Texte zu Antike und Christentum / Studies and Texts in Antiquity and Christianity, 62),